AGIZO: JPM atoa siku 14 wamiliki vituo vya mafuta kufunga mashine za EFDs, watakao kaidi kufutiwa leseni ya biashara...# share

Rais John Magufuli ametoa siku 14 kwa wamiliki wa vituo vya mafuta nchini, kuhakikisha wanaweka na kutumia mashine za kielektroniki (EFDs) na atakayeshindwa kutekeleza  agizo hilo atafutiwa leseni ya biashara.


Rais Magufuli akiweka jiwe la msingi leo katika ufunguzi wa barabara ya Kigoma-Biharamulo-Lusahunga yenye urefu wa Kilometa 154.

Kauli hiyo imetolewa leo na Rais Magufuli wakati akiweka jiwe la msingi katika ufunguzi wa barabara ya Kigoma-Biharamulo-Lusahunga yenye urefu wa Kilometa 154.
Aidha amewataka Mawaziri wenye dhamana kuhakikisha wanafuatilia  agizo halo kuanzia sasa ili litekelezwe kikamilifu.

"Wanaolalamika kukosa mafuta waendelee kufanya hivyo, ni mara mia tukose mafuta kuliko kuwa na wafanyabiashara wanaokwepa kodi", amesema Rais Magufuli.

Kwa upande mwingine, Rais Magufuli amepiga marufuku wananchi kutozwa kodi kwa mzigo wenye uzito wa tani moja anapousafirisha kutoka wilaya moja kwenda nyingine.

Rais Magufuli ameanza ziara ya siku mbili katika Mkoa wa Kagera ambako mbali na kuongea na Wananchi, na kufungua miradi ya maendeleo ambapo amenza kwa uzinduzi wa jiwe la msingi katika barabara ya Kagoma-Biharamulo-Rusaunga yenye urefu wa kilomita 154 iliyojengwa kwa kiwango cha lami ambayo imegharimu sh. bilioni 190.4.

Anatarajia katika ziara hiyo pia kufika katika mikoa ya Kigoma, Tabora na Singida ambako atafungua na kuzindua miradi 9 kati ya Julai 19 hadi 25.
Na Mwandishi Wetu


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search