NEWS: Waziri Ummy amekuja na kauli hii kukabili changamoto kwa watoto wa kike shuleni....# share


WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amewasa watoto wa kike wa shule mbalimbali  nchini kutafakari matokeo ya mwaka huu ili kuwa chachu ya kujitambua na kujikinga na mimba shuleni.


Kauli hiyo imetolewa na Waziri Ummy katika tarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini cha wizara hiyo yenye lengo la kuwapongeza watoto wa kike kwa ufaulu mzuri katika mtihani wa kidato cha sita mwaka huu.

Amesema kama wanafunzi wa kike watajitambua watasoma kwa ari kubwa kwa manufaa yao na Taifa kwa ujumla. 

Aidha taarifa hiyo imebainisha kuwa Ummy amempongeza Sophia Juma wa shule ya Sekondari Mazinde juu (Tanga) kwa kushika nafasi ya kwanza pamoja na Agatha Ninga wa shule ya Wasichana Tabora ambaye ameshika nafasi ya pili kitaifa.
   
Kwa mujibu wa tarifa hiyo pia amewapongeza wanafunzi wote wa kwa jitihada walizoonesha na   kuweza kufaulu mitihani yao kwa kiwango cha asilimia 97.21 ya waliofanya mtihani, ikilinganishwa na asilimia 95.34 ya wavulana waliofaulu.

Waziri ameeleza kufarijika na juhudi   ya wanafunzi wa kike, kufuatia ufaulu wa daraja la kwanza hadi la tatu na kupanda kwa asilimia         94.07 katika madaraja haya ikilinganishwa na wavulana waliofaulu kwa asilimia 93.49.

Amebainisha kwa kusema kuwa juhudi hizo sio za kubezwa ambapo alisema kwamba ni ishara thabiti kuwa mtoto wa kike akipewa nafasi  anaweza.
 
Amesema wizara inatambua ushirikiano wa walimu, wazazi, na jamii ambao wamewezesha kufikiwa kwa ubora wa ufaulu wa watoto wa Kike ambapo alibainisha kuwa juhudi zao ndizo ambazo zimesaidia utekelezaji wa azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kutoa fursa sawa kwa watoto wa kike na wa kiume katika kupata haki ya elimu.


Ametoa rai kwa watoto hao wakike waelewe kuwa wamehitimu daraja moja, hata hivyo bado wanalojukumu la kujiendeleza zaidi katika taaluma mbalimbali kama njia ya kumwezesha        mtoto wa kike na mwanamke kuchangia katika maendeleo ya taifa kwa umahiri mkubwa.  

Mwandishi Wetu

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search