AGIZO: Waziri Mwakyembe aivaa Startimes.. #share.. aiundia 'kikosikazi' cha watu kumi...
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo,Dk. Harrison
Mwakyembe amesema ameunda kamati ndogo ya watu 10 kuhusiana na agizo la Rais
Magufuli la Kampuni ya Star Media, ambapo majibu yatapatikani ndani ya siku
saba.
Akizungumza Dar es Salaam, leo baada ya kumaliza kikao na
Mwenyekiti wa kampuni hiyo Xinxing Pang, alisema baada ya agizo la Rais walikaa
Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Mamlaka ya Mapato Tanzania (TCRA) pamoja
na wizara yake kupitia masuala mbalimbali ndipo walipofikia uamuzi wa kuunda
kamati.
Alisema kamati hiyo imeundwa na watu watano kutoka Tanzania
na watano kutoka kwao, ambapo kwa kipindi hicho naye Mkaguzi Mkuu wa Hesababu
za Serikali (CAG) alikuwa anamalizia uchunguzi wake.
“Sula hili hatutaki lichukue muda mrefu, tunataka liishe
mwezi huu, ambapo majadiliano yatakayopatikana kwenye kamati hiyo nitampigia
simu Mwenyekiti kumueleza tulipofikia. Kwa sababu tayari sisi tulikuwa na
msimamo wetu.
“Ndiyo maana aliamua kuja kutoka China ili kujua moja kwa
moja kuhusiana na msimamo wetu na kuwa kwa nini Kampuni yao haileti faida,”amesema
Dk. Mwakyembe.
Alifafanua kuwa makubaliano hayo ya kuunda kamati yalifikia
baada ya kukaa nao katika mazungumza na wao wakatoa sababu zao ndipo walipofikia
uamuzi huo wa kamati ili kujua nini ambacho kinasababisha faida isipatikane.
Alibainisha kuwa kwa hatua hiyo agizo la Rais Magufuli
limefanyiwa kazi na wakishamaliza kushughulikia suala hilo watampelekea taarifa
rasmi za uchunguzi wa kina.
Hata hivyo, akifafanua kuhusu ripoti ya CAG alisema
wanategemea kupata ripoti hiyo muda wowote kuanzia sasa, hata wao bado
hawajaisoma, kwa sababu wanataka jambo hilo lifanyiwe kazi haraka waliamua
kufanyia kazi mkataba wa makubaliano.
“Tunataka jambo hili limalizike mapema ndiyo maana tukaamua
kushughulika kwanza na mkataba na hiyo ripo ya CAG yenyewe itasaidia yale
majadiliano yatakayopatikana kwenye kamati ndiyo maama tumeipa kamati siku saba
tu,”alisema
Dk. Mwakyembe alisema kama timu hiyo haitamaliza kazi yao kwa
wakati kwa kudhani kuna suala la msingi imeliacha, itaongezewa siku mbili au
tatu iweze kulikamilisha kutokana na umuhimu wa suala hilo.
Kwa upande wake, Mwenyekiti huyo, amesema amekuja nchini kwa
sababu ya maswali kadhaa yaliyotolewa na Rais Magufuli kutokana na Kampuni yao,
kwa hiyo wamezingatia maswali hayo na watayafanyia kazi.
“Tunafanya juhudi nyingi za kujibu maswali hayo na ndiyo
maana nimekuja kuzungumza na Waziri na kutoa mrejesho wa kazi tuliyofanya
za Star Media na pia tunatafuta sababu ambazo Kampuni yetu inatupa hasara na
njia ya kutupa faida baadaye,” alisema
Na Abraham Ntambara
No comments:
Post a Comment