Press Release:TCRA yazishushia rungu kampuni za simu, yazipiga faini kwa kusajili laini bila vitambulisho…# share


MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imezitoza faini kampuni zote za simu nchini kwa kosa la kusajili laini bila vitambulisho na kutofuata utaratibu.


Hayo yalibeinishwa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mkuu wa TCRA James Kilaba akizungumza na waandishi wa habari, alisema hii si mara ya kwanza kwa kampuni hizo kutozwa faini kwa kukiuka sheria.

Alitaja kampuni hizo na viwango vya faini, alisema Airtel sh. biloni 1.08, Smart sh. bilioni 1.3, Vodacom sh. milioni 945, Zantel sh. milioni 105 na Halotel sh. bilioni 1.6.

“Kutokana na kwamba zimerudia kosa tumeziongezea faini tena, Airtel imetozwa sh. milioni 542, Smart sh. milioni 37, Tigo sh. milioni 625, Zantel sh. milioni 52 na Halotel sh. milioni 822,” amesema.

Pia, kampuni hizo zimetozwa Sh. milioni 500 kila moja kwa kosa la kuathiri na kuhatarisha usalama wa umma na jamii ya Watanzania kwa kusajili laini bila kufuata utaratibu.
Na Mwandishi Wetu



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search