bREAKING nEWS: Haya Hapa Mashtaka aliyosomewa Lissu.. mwenyewe akana,.. hoja ya dhamana inaendelea kujadiliwa.. #share

Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni Tundu Lissu, amepandishwa kizimbani mchana huu na kusomewa mashtaka ya kutoa lugha ya uchochezi dhidi ya Serikali ya Awamu ya Tano, katika maeneo ya Ufipa, Kinondoni.. mnamo siku ya Julai 17, 2017 


Katika hati ya Mashtaka, inadaiwa kuwa maneno hayo yalikuwa na lengo ya kuleta chuki dhidi ya viongozi ndani ya Jamuhuri ya Tanzania.


Lissu amepandishwa mahakamani hapo , mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu,Wilbard Mashauri, na amekana shtaka hilo..



Hata hivyo, upande wa mashtaka wameomba mahakama anyimwe dhamana huku upande wa utetezi wakipinga hoja hiyo.



Kumekuwepo na mvutano mkali juu ya dhamana ya Lissu, ambapo Mahakama imeamuru arudishwe rumande hadi siku ya Tarehe 27 atakaporudishwa tena Mahakamani..



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search