Exclussive ya Giggy Money na Bosi wa WCB: "Subirini muone matokeo.." #share

Chipukizi anaepasua anga za Bongo na medani za starehe za Dar, Gigy Money.. amezidi kufunguka na kuonyesha kutekwa kwake kihisia na kiranja wa bongo fleva ambae pia ni bosi wa lebo ya Wasafi "WCB" Nassib Abdull ‘Diamond Platnumz’.. 


Giggy hapa akiwa sambamba na Rich Mavoko enzi zileee !!
Akinukuliwa 'kwenye maongezi 'na mtandao wa Jamboleo online, Giggy alitonya.. 'mahesabu yote yamekamilika na ninachokifanya kwa sasa ni kuweka sawa mtego kwa kumnasa rasmi...' 

Katika siku za karibuni katika mitandao ya kijamii kumeonekana kusambaa kwa kasi kubwa kwa picha zinamuonesha Gigy Money akiwa na Diamond wakiwa kwenye mandhari tofauti-tofauti. 

Katika ya interview aliyofanya na mmoja wa watangazaji maarufu wa redio hivi karibuni, Gigy alisema watu wasubiri kuona matokeo kwani mengine ni siri na hayupo tayari kumwaga mtama hadharani.. 

Gigy amesisitiza katika safari yake ya kumnasa Chibu yuko ‘serious’ kabisa na kawaida kumpenda mtu akikubali kuwa mateka basi anatekwa. “Wangapi wanaonekana kama washapita tu, yeye mwenyewe mbona yupo tayari sema ntakuwa kama natoa siri,”.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search