News Updates:: Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA Tundu Lissu amefikishwa Mahakamani mchana huu.. #share

New Updates:: Mwanasheria wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani Bungeni.. Tundu Lisu, amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mchana huu kujibu mashtaka yake ambayo bado hayajawekwa wazi.

IMG-20170724-WA0007.jpg
Wakati Lissu akifikishwa Mahakamani, kuna taarifa za makada sita wa CHADEMA ambao amekamatwa eneo la Kituo cha kati cha Polisi wakati wakifuatilia yanayojiri tokea kukamatwa kwa Rais huyo wa TLS ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki,

Hapo awali, afisa Habari wa Chadema Tumaini Makene, alibainisha uwepo wa uwezekano wa Lissu kupanda kizimbani kufuatia mazingira tofauti yanayohusiana na kukamatwa kwake..

Endelea kufuatana nasi kupitia www.matukio360.com kupata yanayojiri kadri ya tutakavyoyapokea...  
 

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search