Heka Heka: Kondakta huko Zanzibar ameuawa kikatili alipokuwa akidai nauli yake..#share

Kondakta mmoja wa daladala mjini Zanzibar amefariki dunia baada ya kupokea kipigo kwa kosa la kupishana kauli na abiria wake baada kumdai nauli. 
Kwa mujibu wa audio clip iliyosambaa sana kupitia mitandao ya kijamii, inaelezea tukio hilo la kutisha na jinsi kondakta alivyopambana kuokoa maisha yake, lakini akazidiwa nguvu na abiria huyo aliekuwa amekusanya 'masela wenzake kibao' katika kutekeleza shambulio hilo..


Nae mpashaji mmoja aliejulikana kwa jina la Bi Amina Mwinyi mkaazi wa mitaa ya jang'ombe, akielezea undani wa tukio lenyewe anasema.. 
Kondakta huyo amefariki baada ya kipigo kikali kutoka kwa 'sela' mmoja ambae alikusanya wenzake na kuamua kuivizia njiani gari hiyo na kisha kumshusha konda na kumshushia kipigo cha 'mbwa mwizi'.. "masikini wamemuua kijana wa watu bila hatia yoyote.. Allah amrehemu.." alimaliza Bi Amina.

Taarifa zinasema, mwili wa marehemu uko hospital na mipango ya mazishi yanayotarajiwa kufanyika leo inaendelea..

Matukio360 tumedaka 'audio' inayoelezea mkasa mzima na tumekushushia hapa chini.. endelea kufuatana nasi tukiendelea kupata undani wa tukio hili kutoka vyanzo husika..

bofya kusikiliza.. 

https://drive.google.com/open?id=0Bwm-EVBD4Wr9RkVNc2Fab2h2QTg


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search