INAUMA SANA..!! Baada ya lile povu la 'kumdetisha Ali Kiba' Queen Darleen sasa kaibuka na siri nzitoo.. #share

Baada ya 'mlipuko mtandaoni' uliozusha fununu za mahusiano kati ya Mkongwe wa Rymes katika anga za Bongo Ali King Kiba na Mrembo nyota mwenye uzuri wake Queen Darleen,.. 


Mwanadada Queen Darleen katika ubora wake.. 
Hatimae mwanadada huyo 
anayefanya vizuri akiwa chini ya Lebo ya ‘WCB’, 'amefunguka' na kumwaga mtama hadharani kuwa anaumizwa sana na hali ya kuishi bila mpenzi jambo ambalo limekuwa likimuumiza sana katika maisha yake ya sasa, maana yeye pia anahitaji kupenda na kupendwa kama walivyo watu wengine.


Akichonga na Showbiz Xtra, Queen Darleen, ambae ni dada wa Boss wa WCB Diamond Platnumz, alisema kuwa,.. tangu aachane na mzazi mwenziye aliyezaa naye mtoto mmoja wa kike, hajawahi kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi jambo ambalo amekuwa akijiuliza bila kupata jibu kuwa linasababishwa na nini...?


“Naumizwa na hii hali,.. kuna wakati huwa nafikiria wanaume wananiogopa au sijui ni kitu gani kinatokea.. sasa nahitaji kuwa na mpenzi,” alisema Darleen - Crdts Bong Movie

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search