Mabawa aja na Kampeni ya 'Magufuli Baki..' Kitaifa.. #share
Mtangaza nia wa nafasi ya Ubunge wa Chama cha Mapindunzi (CCM), Jimbo la Segerema katika Uchaguzi mkuu uliopita Bw. Laurence Mabawa, amewataka Watanzania kujitokeza kwa wingi katika kupokea Kampeni ya "Magufuli Baki" yenye lengo la kumpongeza, Rais John Magufuli kwa kazi anayoifanya na kupata maoni kutoka kwa wadau mbalimbali juu ya utendaji kazi wa utawala wa awamu ya tano(5).
Akiongea na waandishi wa Habari kwenye Ofisi za Idara ya Habari Maelezo leo, Bw. Mabawa amelaani vikali kauli na matamko yanayotolewa na baadhi ya Wanasiasa Nchini juu ya nia njema ya kampeni hiyo yenye lengo la kumpongeza Rais na Serikali yake,.. akiongeza kuwa Watanzania wanatambua kazi kubwa inayofanywa na Rais Magufuli ya kutetea na kupigania rasilimali za Taifa na Maslahi ya wananchi masikini wa Taifa hili zinazofanywa na serikali yake...
"Mimi kama Mtanzania mzalendo nimeamua kuchukua jukumu la kuanzisha kampeni ya "Magufuli Baki" kwa lengo la kupata maoni juu ya wananchi kuhusu utendaji kazi wa Rais," alisema Mabawa.
Alisema kampeni ya Magufuli, itahusisha Mikoa yote ya Tanzania kwa kuwafikia Wananchi na kufanya nao mikutano yenye nia njema ya kumuuombea Rais abaki katika msimamo wake wa kutetea Taifa.
Ameeleza kuwa kampeni hiyo inatoa fursa kwa wananchi kutoa maoni ya utendaji kazi wa Serikali kwa ujumla kupitia mikutano na mitandao ya kijamii maalum iliyoandaliwa na kampeni hiyo.
"Pia nawaomba Wanasiasa kuacha kutoa maneno ya makali na ya kuudhi yenye kumpinga Rais kwa kile anachokifanya..."alisema Mabawa.
No comments:
Post a Comment