ONYO: Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani halitakuwa na msamaha kwa madereva wavunjifu wa sheria kwa mwanvuli wakutopewa elimu..#share


JESHI la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani nchini limesema halitasita kutoa adhabu kwa madereva wanaovunja sheria za usalama barabarani kwa kisingizio kuwa hawana elimu juu ya makosa hayo na pia kutoelezwa sababu za kukamatwa.


Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Jeshi hilo Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi  Fortunatus Musilimu, akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano ulioitishwa na wizara ya mambo ya ndani uliokuwa na lengo la kuuarifu umma kuwepo kwa tamasha kubwa Agosti 5 mwaka huu lilioandaliwa na Baraza la Usalama Barabarani Taifa.

Aidha ameeleza kuwa taratibu na sheria za jeshi hilo zinamtaka polisi anapomkamata mtu kumwelezak sababu za kumkamata kwa kutaja kosa lake.  

“Lazima ajulishwe tatizo lake, ndiyo sehria inavyosema, lakini nachotaka kusema na niwe muwazi kabisa kuna baadhi ya madereva ambao makosa ya usalama barabarani wanayachukulia kama ni makosa madogo madogo ya kuchezea chezea wanafanya mzaha, mzaha ambao unapelekea kutokea kwa ajali ambazo ndizo zinasababisha vifo vya watu,”

“Wewe ni dereva umepata mafunzo ya udereva unategemea tukupe elimu gani barabarani, unategemea tukupe elimu gani barabarani?, sasa nasema hivi kwa dereva anayetegemea akamatwe amefanya kosa tumpe elimu barabarani hilo hatutafanya kama unetegemea kupata hiyo elimu barabarani ni afadhali usiingize gari lako barabarani kwani hatutafanya hivyo na tutakuchukulia hatua pale pale,” alisema Kamishna Musilimu.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Hamadi Masauni ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Usalama Barabarani Taifa akizungumzia tamasha hilo lililoandaliwa, amesema ni mkakati wa awamu ya pili katika kupunguza ajali za barabarani.

Amesema lengo la tamasha hilo  ni kutoa elimu kwa wadau mbalimbali wa usafiri ili kupunguza au kuondoa tatizo la la ajali. Alitaja wadau hao kuwa  ni pamoja na watumiaji wa usafiri, wamiliki wa vyombo vya usafiri, madereva na wananchi.

Aidha amesema kuwa mgeni rasmi katika tukio hilo anatarajiwa kuwa Rais John Magufuli. 

Na Abraham Ntambara

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search