Sports news; Cheko, Nderemo na vifijo.. Kamati ya TFF ikimuachia huru Haji Manara #share

Kamati ya Nidhamu ya TFF imemfutia adhabu ya kutojihusisha na soka kwa mwaka mmoja Afisa Habari Simba, Haji Manara. 


Taarifa ya kina iliyapatikana kutoka vyanzo vya kuaminika zinasema, Haji hivi sasa yuko huria kuendelea na majukumu yake kama msemaji 'vuvuzela' wa simba..

Matukio360 tunaendelea kuwajuza yanayojiri klabuni Mzimbazi na kwa mtani Jerry Muro mara baada ya kuvuja kwa 'tetesi' hizi..

Itakumbukwa mara baada ya kufungiwa, haji aliijia juu kamati ya nidhamu ya TFF kwa maamuzi aliyoyaita ya kionevu na kuapa kutetea haki yake kwa 'jasho na meno..'

Kupitia ukurasa wake wa instagram, manara pia alibainisha kwamba wakati wa maamuzi ya TFF alikuwa Zanzibar kikazi na akashangazwa na uharaka uliojitokeza.. na maamuzi bila ya yeye mlalamikiwa kusikilizwa..



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search