sPORTS nEWS: UEFA yaishushia rungu kali Manchester United, pia yafungia wawili....#share

Chama cha Soka Barani Ulaya (UEFA) leo kimetangaza kumfungia mchezaji mwingine wa
klabu ya ‘Mashetani Wekundu’ Manchester United Phil Jones mechi mbili, kwa kosa la kukataa kuchukuliwa vipimo
vya utumiaji wa dawa zisizoruhusiwa michezoni na kuendelea kufurahia na wenzake
ubingwa wa Europa.
Adhabu hiyo
imekuja baada ya siku kadhaa toka beki wa kimataifa wa Ivory Coast anaekipiga na klabu
hiyo Eric Baily kufungiwa
michezo mitatu na chama hicho.
Aidha adhabu
hazikuishia kufungiwa mechi tu bali pia wote wamelimwa faini ya pauni 4500 kwa
kosa hilo la kwa makosa hayo ya utovu wa nidhamu kwa waliyotenda kwa maofisa wa
UEFA.
Aidha Adhabu ya UEFA haikuishia
kwa wachezaji hao bali club pia ya Man
United imepigwa faini ya pound 8,900 kwa kuvunja sheria kwa
kushindwa kuhakikisha wachezaji wake wanapima.
Pamoja na rungu hilo UEFA imewapa Man United siku tatu za kukata
rufaa dhidi ya adhabu hiyo.
Chanzo: Sport360
Chanzo: Sport360
No comments:
Post a Comment