bREAKING sPORTS: Yametimia Simba sasa kumilikiwa na Bilionea Mo-Dewji.....#share

Klabu ya Simba imepitisha rasmi mabadiliko mapya ya uendeshaji wa klabu hiyo kuelekea kwenye mfumo wa hisa ambao kila mwananchama anaweza kuwekeza hisa katika klabu hiyo.


Hayo yameafikiwa leo katika mkutano mkuu wa wanachama wa klabu hiyo uliofanyika Jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere.

Awali akihutubia katika mkutano huo Rais wa Simba Salum Abdalla amesema lengo la klabu ya Simba ni kuwa na shule ya michezo (Academy) viwanja vya michezo na usajili mkubwa.

"Kukaribisha wawekezeji si kuuza timu, kuna utaratibu unawekwa wa uwekezaji lakini sio kuuza timu kama ambavyo wengi wanadhani,” amesema


Klabu ya simba itakuawa na uwezo kuboresha muundo wa kiutawala na kujiwezesha kitaalmu, itaweza, kulipa mishahara, kutengeneza Academy na miundombinu mingi inayo hitajika katika klabu kubwa kama Simba"- katibu wa kamati ya mabadiliko bwana Selemani.


Bilionea Mo amekuwa akihitaji kwa muda mrefu kuwekeza katika klabu hiyo kwa kumiliki hisa asilimia 51 huku 41 wakimilki wanachama. Hivyo hatua hiyo iliyofikiwa leo ni ishara kuwa sasa matamaniyo yake yanakwenda kutimia.

Na Mwandishi Wetu

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search