gOOD nEWs: CAMEL OIL nao wajitosa kusapoti juhudi za RC Makonda kuinua Sekta ya Afya Jijini Dar es Salaam.. #share


NEEMA SEKTA YA AFYA MKOA WA DAR ES SALAAM.

 


Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mheshimiwa Paul Makonda leo amepokea Vitanda 150 na Magodoro 150 vyenye tamani ya zaidi ya shilingi Million 300 kutoka kampuni ya mafuta ya Camel Oil iliyoamua kuunga mkono juhudi za Mkuu wa Mkoa katika kuboresha sekta ya Afya.

Akizungumza baada ya kupokea Vitanda hivyo, Makonda amesema amedhamiria kuhakikisha changamoto zote zinazoikabili sekta ya Afya katika Mkoa wa Dar es Salaam zinamalizika lengo likiwa ni kuhakikisha Wananchi wanapata huduma bora za afya.

“Sitaacha kutafuta kwa ajili ya Wananchi wa Dar es salaam, nitabisha hodi kila panapostahili ilimradi Wananchi wangu wawe wanapata huduma za Afya katika mazingira mazuri. Na siku moja waone kazi kubwa inayofanywa na Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dr. John Magufuli. Sisi tunataka Maendeleo na maendeleo hayana chama,dini wala kabila. Jukumu la kuuendeleza Mji huu wa Dar es salaam ni jukumu letu sote kama wakazi na wananchi wa mkoa huu” Alisema Makonda.

Makonda amesema anatamani siku moja kila mama anaekwenda kujifungua alale kitanda kimoja mwenywe na sio kama ilivyo sasa ambapo wanatumia kitanda kimoja kina mama watatu hadi wanne

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search