gOOD nEWS: Polisi yaua 13 Kibiti katika majibizano ya risasi....#share


WATU 13 wameuawa katika majibizano ya risasi baina yao na polisi katika eneo la Tangibovu, kijiji cha Miwaleni Kibiti mkoani Pwani.


Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro akielezea baadhi ya vitu mbalimbali vilivyokuwa vikitumiwa na wahalifu 13 waliouawa katika eneo la Tangibovu, kijiji cha Miwaleni Kata ya Mchukwi, Tarafa ya Kibiti.

Taarifa kutoka ndani ya Jeshi hilo zinaeleza kuwa baada ya upekuzi, polisi walikamata bunduki nane aina ya SMG pamoja na vifaa vingine.

Kuuawa kwa watu hao ni mfululizo wa operesheni inayofanywa na Jeshi la polisi kuwasaka watu waliokuwa wakifanya mauaji ya viongozi wa Serikali za vitongoji, askari wa Jeshi la Polisi na wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM), ambapo mpaka sasa zaidi ya watu 37 wameshauawa kwa kupigwa risasi.

Jana picha zilizotumwa na jeshi hilo katika vyombo vya habari zinamuonesha Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Simon Sirro akipata maelezo kutoka kwa Mkuu wa Operesheni Maalumu za Jeshi la Polisi, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Liberatus Sabas kuhusu mauaji hayo.

Katika tukio hilo, mbali na silaha nane pia zilikamatwa risasi  158, pikipiki 2, pamoja na  begi la nguo  vilivyokuwa  vikitumiwa na wahalifu hao.

Baada ya kukagua vifaa vilivyokamatwa, IGP pia alizungumza na baadhi ya wananchi wa Kibiti na kuwahakikishia usalama wa maisha na mali zao.





Na Mwandishi Wetu

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search