Kutoka Mahakama Kuu: Profesa Lipumba na Kundi lake wakwaa kisiki cha ruzuku, Jaji awapiga chini...#share

MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi CUF anayetambuliwa na ofisi ya Msajili wa Vyama vya siasa, Profesa Ibrahim Lipumba na kundi lake wamekwama mahakamani leo baada ya Jaji Ndyansobera kukataa maombi yake na kundi lake.



Jaji Ndyansobera amekataa kufuta kesi Namba 28/2017 kama ilivyoombwa na Lipumba ili wapate Ruzuku ya Chama  Cha Wananchi wa CUF inayofikia shilingi billion moja na million mia nne toka Julai mwaka jana.

Naibu Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CUF, Mbarala Maharagande amesema kwamba kufuatia uamuzi huo wa mahakama, Profesa Lipumba hataweza kuchukua haa shilingi moja.


Na Mwandishi Wetu

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search