Kutoka Mahakamani Kisutu:Bilionea Yusuf Manji hakufika mahakamani leo kisa...anaumwa!! #share

MFANYABIASHARA na Mmiliki wa Makampuni ya Quality Group Yusuf Manji, ameshindwa kufika katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam kwenye kesi ya tuhuma za Uhujumu uchumi inayomkabili kwa kuwa ni mgonjwa.


Taarifa hiyo ilitolewa jana Wakili wa Serikali, Estazia Wilson mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mwambapa kwamba amepata taarifa kutoka kwa askari Magereza kuwa Manji anaumwa na amepewa siku mbili za kupumzika.

Baada ya Wilson kuieleza hayo, Hakimu Mwambapa aliahirisha kesi hiyo hadi Agosti 25 mwaka huu kwa kutajwa. Hata hivyo, Wilson alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika, akaomba tarehe nyingine ya kutajwa.

Licha ya Manji kutofika mahakamani kwa sababu za kiafya, washitakiwa wenzake Deogratius Kisinda, Abdallah Sangey na Thobias Fwere walifika mahakamani hapo kama ilivyoelekezwa na Mahakama .

Awali, Mahakama hiyo ilikataa kutoa kibali kwa upande wa mashitaka kumchukua Manji kwenda kuhojiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania ( TRA), kuhusiana na masuala ya kodi.
Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Cyprian Mkeha alisema hawezi kuruhusu ombi hilo kwa sababu kesi iliyopo mbele yake ni ya uhujumu uchumi ambayo haihusiani na masuala ya kodi.

Katika mashitaka yanayomkabili Manji na wenzake Inadaiwa Juni 30, mwaka huuu maeneo ya Chang’ombe A wilayani Temeke Dar es Salaam, washitakiwa wote kwa pamoja, walikutwa na askari polisi wakiwa na mabalo 35 ya vitambaa vinavyotumika kutengenezea  sare za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) vyenye thamani ya Sh milioni 192.5.

Ilidaiwa kuwa Julai Mosi mwaka huu, maeneo ya Chang’ombe A, wilayani Temeke, Dar es Salaam, washitakiwa  wote walikutwa na askari polisi wakiwa na mabalo nane ya vitambaa vinavyotumika kutengenezea sare za JWTZ vyenye thamani ya Sh milioni 44.

Katika mashitaka ya tatu, inadaiwa Juni 30, mwaka huu maeneo  ya Chang’ombe A, washitakiwa walikutwa wakiwa na mhuri wa JWTZ ambao uliandikwa ‘’Mkuu wa Kikosi 121  Kikosi cha JWTZ’’ bila kuwa na uhalali kitendo kinachohatarisha usalama wan chi.

Pia inadaiwa, terehe hiyohiyo maeneo ya Chang’ombe washitakiwa walikutwa na mhuri uliokuwa umeandikwa ‘’Kamanda Kikosi 834 KJ Makutupora Dodoma bila kuwa na uhalali kitendo kinachohatarisha usalama.

Na Mwandishi Wetu


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search