Mwanadada aliewahi kuzua 'utata wa jinsia' Caster Semenya aendelea kutamba Mashindano ya Riadha Duniani, ashinda dhahabu 800m.. #share

Mwanariadha wa Afrika Kusini Caster Semenya alishinda dhahabu katika mbio za 800m upande wa wanawake siku ya mwisho ya mashindano ya ubingwa wa riadha duniani jijini London.



Bingwa huyo wa Olimpiki aliandikisha muda wa dakika moja na sekunde 55.16, muda wake bora zaidi na muda bora zaidi duniani mwaka huu.

Francine Niyonsaba wa Burundi alishinda fedha naye Ajee Wilson wa Marekani akachukua nishani ya shaba, wote wawili wakizidiwa na kasi ya kushangaza ya Semenya mita 50 za mwisho katika mbio hizo.
Mkenya Margaret Nyairera Wambui alimaliza wa nne.

Semenya, 26, amesema sasa anapanga kuvunja rekodi ya dunia ya mbio za mita 800 ambayo ni dakika moja na 53.28.

Rekodi hiyo iliwekwa na Jarmila Kratochvilova wa iliyokuwa Czechoslovakia mwaka 1983.
"Tunahitaji kuondoka kwa 1:55 kwanza na itahitaji mazoezi makali sana," amesema.

"Nina mataji ya Olimpiki, dunia na Jumuiya ya Madola kwa hivyo sasa pengine ni wakati wa kuangazia rekodi ya dunia. Ndicho kitu kinachofuata sasa kwenye orodha. Ninajua kwamba itakuwa vigumu lakini nitajaribu hivi karibuni, pengine."

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search