nEWS: ATCL kubeba mizigo na vifurushi vya TPC.....#share
SHIRIKA la Ndege la Tanzania (ATCL) limeingia mkataba wa
miaka miwili wa Makubaliano ya ushirikiano ya kutoa huduma na Shirika la Posta
nchini (TPC) wenye lengo la kuboresha huduma zitolewazo na shirika hilo.
Akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa ATCL, Ladislaus Matindi alisema wameamua kusaini mkataba huo na shirika la posta kwa kuwa shirika hilo tayari lina wigo mpana wa utoaji huduma huku akisisitiza watatumia baadhi ya ofisi za TPC kufanikisha shughuli zao.
“Tunasaini makubalinao ya kutoa huduma na Posta kutokana
wenzetu tayari wameshajijenga wana vituo vingi vya utoaji huduma tunaamini
mizigo na vifurushi havitatumia muda mwingi kufika mahali husika,” amesema
Matindi.
Amesema watashirikiana na shirika hilo kwenye masuala ya
masoko na biashara huku akibainisha TPC tayari wana mtandao mpana ambao
utaifaidisha ATCL.
Amesisitiza kuwa kwa sasa shirika hilo linatoa huduma ya
usafiri kuelekea mikoa ya Dodoma, Tabora, Kilimanjaro, Mtwara, Mbeya, Tabora,
Mwanza huku akiongeza kupitia ushirikiano huo itasaidia huduma kufika haraka
kwenye mikoa inayopakana.
Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TPC, Deo
Kwiyukwa alisema baada ya kusaini mkataba huo wateja wanaotumia huduma ya posta
wataweza kusafirisha mizigo na vifurushi kwa kutumia ndege za ATCL kwa gharama
nafuu.
Kwiyukwa amesema wafanyakazi wa TPC watatumia huduma ya
shirika hilo pale panapohitajika kutoka sehemu kwenda nyingine yote katika
kuharakisha huduma kwa wateja.
Amefafanua kuwa mkataba huo una tija kwa kuwa utasaidia
kuongeza usalama wa mizigo na vifurushi vitakavyosafirishwa na ATCL.
Pia amesema mkataba waliyoingia kwa kiasi kikubwa utasaidia
kupanua masoko yao hasa hasa kwa yale maeneo yaliyokuwa magumu kufikiwa kwa
urahisi.
Amebainisha kuwa baadhi ya majengo ya TPC yatakodishwa na
shirika hilo naa kwamba yatapokodishwa itasaidia kulingizia mapato shirika
hilo.
Na Abraham Ntambara
No comments:
Post a Comment