nEWS: Lema 'awatemea cheche' viongozi wa dini nchini....Adai wanajifanya hawaoni kinachoendelea...Awataka wachukue hatua....#share
Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema amewataka viongozi wa dini nchini kuna kuwa wanawajibu wa kukemea vitendo vya udhalilishari wanavyofanyiwa wabunge wa upinzani.
Kauli hiyo ameitoa leo Mjini Arusha wakati akizungumza na
waandishi wa habari huku akitoa rai kwa viongozi hao kutokemea tu matumizi ya viroba
na bia.
Amesema kwa kusema kuwa viongozi wa dini mbalimbali nchini
wasifumbe macho yao na kujifanya hawayaoni mateso wanayopata viongozi wa
upinzani nchini.
"Viongozi wetu wa dini wasijifanye hili tunalofanyiwa upinzani hawayaoni. Kazi ya viongozi wa dini siyo kukemea bia na viroba bali wanatakiwa wapige kelele kwenye ukiukwaji wa misingi ya sheria inayoendelea hapa nchini dhidi ya upinzani", amesema Lema.
"Viongozi wetu wa dini wasijifanye hili tunalofanyiwa upinzani hawayaoni. Kazi ya viongozi wa dini siyo kukemea bia na viroba bali wanatakiwa wapige kelele kwenye ukiukwaji wa misingi ya sheria inayoendelea hapa nchini dhidi ya upinzani", amesema Lema.
Aidha Lema ameongeza kuwa viongozi wa dini endapo watasimama
katika kukemea maovu yanayofanywa ndani ya nchi yakiwepo ya unyanyasaji
watakuwa wamelikomboa taifa kwenye machafuko.
"Ipo siku kuna watu watashindwa kuvumiliwa haya
tunayofanyiwa, hapo ndipo vita vya wenyewe kwa wenyewe vitakapokuja hapo siku
za mbeleni" amesema.
Na Mwandishi Wetu




No comments:
Post a Comment