sPORTS nEWS: Kauli ya Kiungo Mpya wa Simba Haruna Niyonzima kwa wenye maswali juu yake baada ya kutambulishwa mapema leo...#share

KIUNGO mpya wa klabu ya Simba, Haruna Niyonzima amesema hana maneno mengi ya kuongea na kwamba majibu ya maswali mengi yanayoulizwa yataonekana uwanjani kuanzia kesho.





Niyonzima amezungumza maneno hayo leo mbele ya Waandishi wa Habari makao makuu ya klabu hiyo alipokuwa akitambulishwa pamoja na nyota wengine Emmanuel Okwi na Nicholas Gyan.

Kiungo huyo ambaye ametokea Yanga baada ya kumaliza mkataba wake mwezi uliopita amesema kwa sasa yeye ni mali halali ya Simba na mambo mengine atajibu uwanjani.
“Mimi ni rasmi mchezaji halali wa klabu ya Simba, sina mengi zaidi ya kuongea kikubwa tukutane uwanjani,” alisema Niyonzima.

Niyonzima, Okwi na Gyan wanatarajiwa kuongeza hamasa ya mashabiki wa Wekundu hao katika mchezo wa kirafiki kesho dhidi ya Rayon Sports ya Rwanda katika Tamasha la Simba Day.


Kila ifikapo Agosti 8, klabu ya Simba hufanya Tamasha ambalo hutumiwa kutambulisha kikosi chao cha msimu pamoja na kutambulisha jezi.




Na Mwandishi Wetu

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search