nEWS: Mkemia Mkuu wa Serikali apiga marufuku wafanyabiashara kuingiza kemikali nchini....#share

OFISI ya Mkemia Mkuu wa Serikali imepiga marufuku wafanyabiashara wa kemikali kujishughulisha na uingizaji wa  bidhaa hizo nchini bila kuwa na hati ya usajili wa shughuli hiyo.


Mkemia Mkuu wa Serikali, Profesa Samweli Manyele ametangaza hatua hiyo leo alipozungumza na waandishi wa habari,ambapo pia alipiga marufuku uingizaji kemikali kabla ya kupata kibali.

“Uingizaji wa kemikali za viwanda na majumbani nchini kutoka nje ya nchi unasimamiwa na chini ya Sheria ya Udhibiti na Usimamizi wa Kemikali (The Industrial and Consumer Chemicals (Management and Control) Act (ICCA), No. 3 of 2003),”alisema.

“Sheria hii katika sehemu ya tatu inamtaka kila anayeagiza kemikali nchini ni lazima awe amesajiliwa kwa kuzingatia kifungu cha 11-28 na awe amepewa hati ya usajili (Certificate of Registration) kama ilivyobainishwa kwenye kifungu cha 29 kabla ya kuanza kujishughulisha na biashara,” alifafanua Manyele.

Amesema, sehemu ya pili ya sheria hiyo ya Mwaka 2015 kanuni ya 3(1) (e) inaelekeza kila mdau wa kemikali aliyesajiliwa na kupata hati ya usajili kuomba kibali ili kupata idhini kabla ya kuingiza mzingo wake nchini.

Manyere amesema wafanyabiashara wengi wamekuwa na utaratibu wa kuagiza mzigo kwanza na inapowasili au kukaribia kuwasili ndipo wanaanza kuomba kibali na wengine kuomba usajili kwa mara ya kwanza. Utaratibu ambao ni kinyume cha Sheria ya ICCA.

Mkemia Mkuu huyo pia amepiga marufuku uingizwaji wa mizigo yenye vifungashio vyenye maelezo ambayo hayako katika lugha ya Kiswahili au Kiingereza ambapo mzigo utakaokuja na maelezo yakiwa kwa lugha tofauti hautaruhusiwa kuingizwa nchini.

Aidha ameeleza mzigo utakaoingizwa bila ya ‘label’ hautaruhusiwa kuingia bali utarudishwa ulikotoka kwani inaleta usumbufu katika kuzihakiki.


Na Abraham Ntambara

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search