nEWS: Viongozi Chadema kuunguruma kesho jijini Dar es Salaam juu ya haya.....#share

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kinatarajia kesho kutoa azimio jingine la Kamati kuu ya Chama iliyoketi Julai 29 hadi 30 mwaka huujijini Dar es Salaam kujadili masuala mbalimbali kuhusu mwenendo wa nchi.


Taarifa iliyotolewa leo kwa vyombo vya habari na Ofisa Habari wa Chadema Tumaini Makene, amesema uongozi wa juu wa chama hicho utazungumza na Umma kupitia vyombo vya habari.

“Uongozi wa juu wa chama kesho, utazungumza juu ya azimio jingine la Kamati Kuu ya Chama iliyoketi Julai 29-30 jijini Dar es Salaam kujadili masuala mbalimbali kuhusu mwenendo wa nchi kwa sasa,” amesem.

Ametaja moja ya azimio litakalozungumziwa ni azimio ambalo lilihusu kuporomoka kwa uchumi wa nchi na hali ngumu ya maisha inayowakabili Watanzania lilitolewa Julai 31, mwaka huu kwa umma kupitia mkutano wa Wahariri/Waandishi waandamizi na uongozi wa juu wa chama hicho.

Na Mwandishi Wetu

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search