Simulizi kali ya SOUDY Brown wa SHILAWADU 'ilivyomkaanga' RC Makonda MCT Report.. #share
REPORI ya Baraza la Habari Tanzania (MCT) imeweka bayana, jinsi mtangazaji Soudy Brown, wa kipindi cha
Shilawadu cha Cloudz, alivyotoa simulizi 'mwanzo mwisho' ya namna Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda
alivyovamia kituo cha Clouds Media Group (CMG) Machi 17 mwaka huu.
Ripoti hiyo iliyozinduliwa leo jijini Dar es Salaam baada ya kufanyika uchunguzi wa tukio hilo ukiwa na lengo la kubaini kama kitendo hicho kilikuwa na ukiukwaji wa uhuru wa habari.
Itakumbukwa Machi 17 mwaka huu Makonda alidaiwa kuvamia kituo
cha CMG akiwa na askari hali iliyopelekewa aliyekuwa Waziri wa Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye kuunda
Tume ili kuchunguza tukio hilo.
Soudy Brown wa Shilawadu ni mmoja
wa wafanyakazi wa CMG waliohojiwa na Tume huru ya watu wa nne ikiongozwa na
Mwanasheria Juma Thomas iliyoundwa na MCT kuchunguza tukio hilo.
Haya ndiyo maelezo ya Soudy Brown
kwenye ripoti hiyo iliyopewa jina la ‘Ripoti ya Uchunguzi wa Uvamizi wa Studio
za Clouds TV’ ukurasa wa Tano (5) katika kipengele ‘Ndani ya Studio’.
Brown aliifahamisha Timu kwamba Makonda
aliwaambia kama hawangeitangaza, wangepewa mojawapo ya adhabu mbili: kifungo
cha miezi sita jela au….(hakutaja adhabu nyingine).
Mtangazaji huyo aliiambia Timu
kwamba, alimwelewesha Mkuu wa Mkoa kuwa, Meneja vipindi alimwelekeza aache
habari ya mwanamke huyo kwa sababu haikuwa na uwiano kihabari kwa vile Askofu
Gwajima ambaye anatuhumiwa hakupatikana kutoa maoni yake.
Akaingia kwenye sehemu ya wahariri akidai apewe ‘kipande’ chenye habari ya ‘yule mwanamke’. Alitoa flash disc(kichoteo), akanakili kilichomo kwenye ‘kipande’ hicho na kuondoka.
Na Mwandishi wetu
No comments:
Post a Comment