sPORTS nEWS: Simba kukipiga na Mtibwa Jumapili, kisha kumwendea Yanga mafichoni....#share


TAARIFA KWA UMMA
Klabu ya Soka ya Simba Jumapili hii ya tarehe 13-8-2017,saa kumi alasiri itashuka kwenye Uwanja mkuu wa Taifa hapa jijini kucheza na Klabu ya Mtibwa Sugar ya Morogoro kwenye mchezo wa kirafiki. 

Mchezo huo ni muhimu kwa pande zote mbili kujiandaa na Ligi kuu ya Vodacom inayotarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi huu. 

Simba pia tutautumia mchezo huo kuiwinda klabu ya Yanga, ambayo tutacheza nayo August 23 mwaka huu, kwenye mchezo wa kugombea Ngao ya hisani.

Baada ya mchezo dhidi ya Wakata miwa hao,Simba inatarajiwa kuelekea Zanzibar kwa ajili ya mawindo hayo
 muhimu. 


IMETOLEWA NA... HAJI S. MANARA
MKUU WA HABARI SIMBA SC 
SIMBA NGUVU MOJA

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search