tREANDING nEWS: Kauli ya kwanza ya Rais Paul Kagame kuhusu Tanzania baada ya kuchaguliwa kuwa Rais wa nchi hiyo kwa mara ya tatu ...#share




RAIS wa Rwanda Paul Kagame ameahidi kuendeleza undugu na ushirikiano baina ya Rwanda na Tanzania kwa ajili ya maendeleo ya wa nchi hizo.


Kauli hiyo ameitoa baada ya kupokea pongezi kutoka kwa Rais John Magufuli kufuatia ushindi wake wa kiti cha urais kwa mara ya tatu.

Rais Magufuli ametoa pongezi hizo kupitia ukurasa wake wa twitter kisha Rais Kagame kushukuru na kutoa ahadi hiyo.

Mawasiliano yao yalikuwa kama inavyoonekena hapa chini.





Rais Kagame ametangazwa jana kushinda kiti hicho kwa asilimia 98 katika uchaguzi uliofanyika juzi. Kagame amekuwa madarakani kwa miaka kumi na saba na kufuatia ushindi huo sasa atahudumu muhula wa tatu wa miaka saba.

Wafuasi wake wanamsifu Kagame kwa kuleta utulivu na maendeleo ya kiuchumi nchini humo baada ya mauaji ya kimbari ya mwaka 1994 ambapo maelfu ya watu waliuaawa, Wapinzani wa bwana Kagame walikuwa ni Frank Habineza na Philippe Mpayimana.

Rais Kagame aliingia madarakani mwaka 1994 wakati kundi lake la waasi lilichukua udhibiti wa mji mkuu Kigali na kukomesha mauaji ya kimbart ambapo watu 800,000 watusi na wahutu wenye msimamo wa wastani waliuawa.

Katiba ya Rwanda ilifanyiwa mabadiliko mwaka 2015 na kumpa Kagame fursa ya kusalia madarakani hadi mwaka 2034.

Na Mwandishi Wetu

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search