tETESI zA uSAJILI bARANI uLAYA: Barcelona yakaribia kumpata mbadala wa Neymar.....#share

On Sunday, Mundo Deportivo imeripoti kuwa Barcelona wametuma ofa yao ya kwanza kwa ajili ya kutaka kukamilisha dili la uhamisho wa Ousmane Dembele.

Tangu taarifa kutoka kuwa Neymar ataihama Barcelona kwenda PSG, Mchezaji huyo wa klabu ya Borussia Dortmund  amekuwa akihusishwa kuhamia Barcelona.

Mshambuliaji huyo wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 20 amecheza dakika 90 katika kombe la German Super Cup baina ya  Borussia Dortmund dhidi ya  Bayern Munich jana.
Katika mchezo huo Dortmund ilipoteza kwa penati. Dembele alitoa pasi ya mwisho kwa Pierre Emerick Aubameyang na kufunga goli la pili.

Aidha taarifa zinaeleza Barcelona imeshafanya makubaliano binafsi na mchezaji huyo ambaye yupo tayari kuhamia klabu hiyo ya nchini Hispania.

Kuondoka kwa Neymar ni dhahiri kwamba  mchezaji huyo atakuwa na namba ya uhakika katika kikosi cha kwanza cha Barcelona.

Aidha Barcelona imemtaarifu Dembele kuwa ni chaguo lao la kwanza kwa ajili ya kuziba pengo la Neymar.

Kikwazo kikubwa katika dili hili ni kwamba klabu ya Borussia Dortmund haipo tayari kumuuza chini ya Euro zinazokaribia milioni 100.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search