uCHAGUZI kENYA: Mbeki aupa tano, aipongeza Serikali na Tume ya Uchaguzi IEBC...#share
NAIROBI- KIONGOZI
wa waangalizi wa uchaguzi kutoka Umoja wa Afrika (AU), Thabo Mbeki, amesema
shughuli ya upigaji kura nchini ilikuwa ya uwazi na wameridhishwa huku matokeo
ya awali hadi jana jioni yakionesha kuwa Rais Uhuru Kenyatta anaongoza kwa kura
8,096,122 dhidi ya 6,695,221 za mpinzani wake, Raila Odinga
Licha ya
upigaji kura kuwaridhisha, Mbeki alisema kulikuwa na changamoto kadhaa kama
vile, kufanana kwa ukaribu zaidi kwa rangi mbili za karatasi ziliyokuwa
zikitumika kupigia kura lakini tatizo hilo lilitatuliwa na maofisa wa tume kwa
kuwasaidia raia kutofautisha rangi hizo..
Kiongozi
huyo ambaye ni rais wa zamani wa Afrika Kusini, ameipongeza Serikali na Tume ya
Uchaguzi na Mipaka Kenya (IEBC) kwa kuhakikisha wafungwa wamepiga kura. Idadi
ya wapigakura nchini humo ni milioni 19.6.
“Tunafahamu
kwamba IEBC bado inahesabu na kukagua matokeo. Shughuli ya uchaguzi bado
inaendelea, hivyo bado ni mapema,” alisema Mbeki na kuongeza;
“Hata hivyo,
waangalizi wa AU wanafurahi kwamba uchaguzi ulikuwa wa amani, siku ya uchaguzi
watu walifika kwa wingi, na waliruhusiwa kupiga kura kwa kufuata taratibu za
uchaguzi Kenya na zinazokubaliwa na AU,” alisema Mbeki.
Aidha, Mbeki
aliongeza kuwa waangalizi hao wanaweza kusema kusema shughuli walizohesabu,
upigaji kura na upeperushaji wa matokeo, vilitimiza viwango vya ubora vya Kenya
na AU.
Alisema
wamepokea malalamiko kuhusu upeperushaji wa matokeo na kutoa mwito kwa wadau
kutumia mifumo wa kisheria iliyopo.
Mbeki alisema
maofisa wa juu kutoka Muungano wa Upinzani nchini (NASA), walikutana na
waangalizi wa AU na kuwapa ripoti kuhusu madai ya udukuzi wa mitambo ya IEBC.
Mara baada
ya maofisa hao kuwasilisha madai hayo, Mbeki alieleza kuwa waliamua kuwahoji
kuwa walipata vipi nyaraka hizo walizokuwa nazo za madai ya udukuzi.
“Maofisa hao
wa NASA walijibu kuwa, walipewa ‘ufunguo’ fulani na IEBC wa kuweza kuingia
kwenye seva. Hata hivyo, tuliwaambia kwamba, kwa kufuata fomu 34A itawezekana
kwa kila mtu kubaini matokeo halisi,” alisema Mbeki.
Upinzani
ulitilia shaka uhalisia wa fomu hizo na kusema katika baadhi ya vituo vya
kupigia kura hawakuwa na maajenti na katika baadhi, maajenti wao walizuiwa
kuingia.
Aidha, upinzani ulisema huenda fomu 34A
katika baadhi ya vituo zilifanyiwa mabadiliko.
Kwa upande mwingine, Mbeki alibainisha
kuwa wao kama waangalizi wa AU hawawezi kuzungumzia madai ya upinzani kwamba
mitambo ya IEBC ilidukuliwa na kuongeza kuwa jukumu lao ni kuangalia shughuli
ya uchaguzi inavyofanyika.
“Sisi si
wachunguzi wa uchaguzi. Iwapo tungeona kitu kikifanywa vibaya, kinyume na
sheria za Kenya na viwango vya AU, basi hapo tungeingilia kati,”
“Katika
baadhi ya visa, NASA wamewasilisha malalamiko kwetu kuhusu uchaguzi, mfano
kupatikana kwa usajili wa wapiga kura na usalama na kusafirishwa kwa maofisa
takriban 40 wa polisi kwenda kwingine,”
“Tuliangazia
hayo, na baadhi tukawapasha IEBC kuhusu malalamisho ya usajili na kuhusu polisi
tukawasiliana na kukutana na Waziri wa Usalama Dkt Fred Matiang'I,” alisema
Mbeki.
Naye mjumbe
wa waangalizi wa Jumuiya ya Madola, Rais wa zamani wa Ghana, John Dramani
Mahama alisema walikutana na Odinga na wajumbe wake na walitoa madai ya
kompyuta za IEBC kuvamia huku wakiwa na nyaraka kama ushahidi wa madai yao,
hata hivyo Mahama alisema nao waliwaeleza kwanza hawana utaalamu wa teknolojia
hiyo, lakini jukumu lao ni kuangalia kama utaratibu mzima wa uchaguzi umefuata
sharia na katiba ya nchi na madai mengine ya ukiukwaji wa taratibu yana
utaratibu wake uliowekwa kwa mujibu wa sharia.
Na Mwandishi Wetu
No comments:
Post a Comment