nEWS: Rwebangira aomba kufika Magogoni kumfunda JPM...#share


MKURUGENZI Mtendaji wa Taasisi wa Taasisi ya Milemine East Refining Salvatory Rwebangira ameomba kuonana na Rais John Magufuli ili amwelezee ujuzi na uzoefu wa zaidi ya maiaka 25 alionao katika masuala ya utafiti wa madini na mimea kwa ajili ya utengenezaji wa dawa za binadamu.


Akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam mkurugenzi huyo alisema katika kipindi chake alichofanya utafiti amegundua masuala mengi kwenye madini yanayoweza kutumika katika viwanda na utengenezaji dawa hizo hivyo kuonana naye itakuwa fursa nzuri ya kumuelezea njia zitakazoisaidia nchi kuinua uchumi wa viwanda.

"Namuomba Rais Magufuli pamoja na shughulli zake kuwa nyingi na finyu akihudumia taifa zima anipatie muda wa kumuona nimshukuru binafsi na kwa niaba ya watanzania, pia nipate nafasi ya kutoa neno langu la ujuzi na uzoefu kutokana na historia yangu ya utafiti," alisema Rwebangira.

Aidha Rwebangira amempongeza Rais Magufuli kwa juhudi zake za kuleta mabadiliko nchini kwani kwa muda mchache aliokaa madarakani amenuunua ndege tatu kwa ajili ya kuboresha usafiri wa anga na kukuza utalii wa nchi.

Amesisitiza kuwa amepunguza idadi ya wafanyakazi hewa na wenye vyeti feki huku akibainisha Serikali ya Awamu ya Tano imeafanya kazi ya kupambana na dawa za kulevya ambazo zilikuwa zikiangamiza vijana.

Pia amesema uongozi wa awamu hii umeboresha huduma ya maji kwani hapo mwanzo lilikuwa suala kero kubwa nchi nzima hivyo imewapunguzia wananchi adha ya kutembea umbali mrefu.
Amefafanua kuwa Serikali inayoongozwa Rais Magufuli imeanza Ujenzi wa Reli ya Kisasa inayoanzia Dar es Salaam hadi Morogoro jambo ambalo limewashangaza hata wazungu.

Katika hatua nyingine, amezipongeza Tume za Kuchunguza Makinikia ikiwemo Kamati ya kwanza iliyoongozwa na Profesa Abdulkarim Mruma na ya pili iliyosimamiwa na Profesa Nehemiah Osoro.

Wakati huo huo, Rwebangira amempongeza Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kwa kufuatilia na kusimamia kwa nguvu azma ya viwanda na uwajibikaji wenye nia ya dhati ya kulirudisha taifa kwenye mstari uliionyooka.


Na Hussein Ndubikile

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search