uCHAGUZI tFF: Selasela Mgombea Umakamu wa Rais aja na Sera ya Soka Bora fursa ya Ajira...#share

MGOMBEA wa nafasi ya Makamu wa Rais wa Chama cha Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Robert Selasela amesema atakapochaguliwa katika nafasi hiyo mkakati wake mkubwa ni kuhakikisha anaisimamia vizuri kamati ya fedha.


Kauli hiyo ameitua leo jijini Dar es Salaam akizungumza na waandishi wa habari, amesema sera yake katika uchaguzi huu ni ‘Soka Bora Fursa ya Ajira’, lengo ni kuufanya mpira kuwa ajira.

Amefafanua kuwa ili mpira nchini uweze kwenda mbele ni lazima kuwepo na usimamizi wa mipango ya fedha na uchumi.

“Nimeamua kugombea  baada ya kujitathimini na kuona nafaa katika nafasi hii, naamini nitaongoza vizuri kamati hii,” amesema Selasela.

Aidha amesema lengo la kusimamia kamati hiyo ni kutokana na kwamba matumizi mazuri ya fedha yatasaidia katika kuwekeza chini na kuinua vipaji ikiwa ni pamoja na kujenga miundombinu ya soka.

Amesema kwa kufanya hivyo itaweza kukuza mpira na pia kutengeneza ajira kwa vijana. Alibainisha akipata nafasi hiyo ataweza kuwa kiungo na serikali pamoja na kumshauri Rais wa TFF katika kuweka mipango mizuri kwa ajili ya maendeleo ya mpira.

Amebainisha pia atahakikisha mpira wa wanawake unakuwa nchini kwani soka la wanawake Afrika Mashariki liko chini. Ameeleza katika hilo atasimamia katika utawala bora ili kufanikiwa.


Aidha amesema katika uongozi wake atashauri TFF kujiimarisha kwanza kisha kushuka chini katika vyama vya mpira vya mikoa na wilaya kwani ndiko vipaji vilipo badala ya kuangalia tu ligi kuu.

Na Abraham Ntambara

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search