ANGALIZO: Kuelekea Mitihani ya Darasa la 7 kesho...NECTA imesema Itavifutia Usajili Vituo Vyote Vya Mitihaini ambavyo...#share

BARAZA la Mitihani Tanzania (NECTA), limesema litavifutia usajili vituo vyote vya kufanyia mitihani ya Darasa la Saba kwa vituo ambavyo wamiliki wake wataingilia majukumu ya wasimamizi wa mitihani inayotarajiwa kufanyika kesho na kesho kutwa yani Septemba 6 hadi 7 mwaka huu.



Kauli hiyo imetolewa mapema leo jijini Dar es Salaam na Katibu Mtendaji wa NECTA, Dk. Charles Msonde wakati akizungumza na waandishi wa habari, amesema wamiliki wanatakiwa kujua kuwa shule zao ni vituo maalumu vya kufanyia mitihani tu.

“Baraza linawataka wamiliki wa shule zote kutambua kuwa shule zao ni vituo maalum vya kufanyia mitihani, hivyo hawatakiwi kwa namna yoyote kuingilia majukumu ya wasimamizi wa mitihani hiyo.

“Baraza halitasita kukifuta kituo chochote cha mitihani endapo litabaini na kuthibitisha pasina shaka kuwa kituo hicho kinajihusisha na udanganyifu wa mitihani.
Aidha ametoa wito kwa jamii kutoa ushirikiano kwa kipindi hiki cha mitihani ili wanafunzi wafanye mitihani yao kwa utulivu.

“Tunawaasa walimu, wamiliki wa shule, wasimamizi na jamii kwa ujumla kutojihusisha na udanganyifu wa aina yoyote. Wataokiuka haya hatutasita kuwachukulia hatua kwa mujibu wa sheria za nchi,” amesisitiza Msonde.


Ameeleza kuwa wanafunzi hao watafanya masomo matano ambayo ni: Kiswahili, Hisabati, Maarifa ya Jamii, Sayansi na English ambapo mitihani hiyo imeshasafirishwa kupelekwa vituoni.

Na Abraham Ntambara

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search