Mfanyabiashara Yusuf Manji, wenzake 3 wahojiwa polisi kwa agizo la Mahakama...Baada ya mahojiano wapelekwa....#share

JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam leo limefanya mahojiano na Mfanyabiashara Yusuf Manji  na Wenzake watatu juu ya tuhuma zinazowakabili za Uhujumu Uchumi kama Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilivyoliagiza Jeshi hilo kumhoji.


Baada ya Jeshi hilo kumaliza mahojiano yao dhidi ya mshtakiwa Manji na wenzake wamewakabidhi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kama ilivyoamriwa Jana.

Mbali na Manji ambaye ni mfanyabiashara maarufu nchini, washitakiwa wengine waliokabidhiwa ni Meneja Rasilimali watu wa Kampuni ya Quality Group Ltd, Deogratius Kisinda, Mtunza stoo, Abdallah Sangey na Thobias Fwere.

Akiwakabidhi watuhimiwa hao, wakili wa serikali mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi kuwa washtakiwa hao wamerudishwa mahakamani kama ilivyoamuriwa, baada ya polisi kumaliza kuwahoji.

Baada ya washtakiwa kukabidhiwa wakiwa salama na afya zao nzuri, Hakimu Shaidi alisema kesi hiyo itaendelea na utaratibu kama ulivyokuwa awali, ambapo itatajwa September 8/2017.

Jana mchana mahakama hiyo iliruhusu Manji na wenzake kwenda kuhojiwa na Polisi  ili kukamilisha upelelezi katika kesi ya uhujumu uchumi.

Na Mwandishi Wetu

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search