Baada ya Manji jana kufutiwa kesi na DPP, Gwajima naye leo aibwaga Jamuhuri Mahakamani Kisutu....#share

ASKOFU Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Josephat Gwajima amefutiwa kesi ya kushindwa kutunza silaha baada ya mahakama kushindwa kuthibitisha mashtaka hayo, na kuamuru arudishiwe mkoba wenye silaha yake.


Akisomewa  kesi hiyo ya mwaka 2015 leo  akiwa na wasaidizi wake watatu, Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam alithibitishia umma kwa kusema kutokana na ushahidi wa upande wa mshitakiwa (Askofu Gwajima) akiulinganisha na ushaidi upande wa Mashitaka(Jamhuri), haoni sababu ya hukumu juu ya Askofu Gwajima.

Hakimu ameitaka Jamhuri kurudisha begi na silaha anayoimiliki Askofu Gwajima mara moja.


Kufutwa kwa kesi hiyo ni ishara kwamba Gwajima ameibwaga Jamhuri.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search