TRL Yafuta Kwa Muda Safari za Treni ya Abiria kutoka Dar es Salaam Kwenda Mwanza na Kigoma...#share

KAMPUNI ya Reli Tanzania (TRL), imefuta safari ya treni ya abiria kwa siku mbili ili kufanya marekebisho ya uboreshaji wa miundombinu ya reli  katika eneo la kati ya stesheni ya Morogoro na Mazimbu kutokana na daraja lililopo katika eneo lenye ukubwa wa  kilimeta 209/7 kuharibiwa na mvua.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Kaimu Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa TRL Focus Sahani, alisema safari zilizofutwa ni ya Septemba 19 treni ya kutoka Dar es Salaam kwenda Mwanza na Kigoma pamoya na ya Septemba 21 mwaka huu  kutoka Kigoma na Mwanza kenda Dar es Salaam.

Aidha ameeleza kuwa daraja hilo lilisombwa na maji ya mvua mnamo Mei 13 mwaka huu majira ya saa 5 usiku na likafanyiwa matengenezo ya dharura tu lakini kwa sasa tathmini ya kiufundi imefanyika na kuthibitisha kuwa ni hatari kuendelea kupitisha treni bila kuimarisha zaidi.

“Uongozi wa kampuni umeona ni muda muafaka sasa kulifanyia marekebisho madhubuti nay a uhakika ili kuhakikisha usalama wa wateja wetu na wananchi kuwa unapewa kipaumbele,” amesema Sahani.

Sahani amebainisha kutokana na hali hiyo na ili kufanya kazi kwa umakini wamelizamika kufanya marekebisho hayo ya ratiba kwa ajili ya kutoa nafasi ya kufanikisha zoezi hilo la kulifanyia matengenezo madhubuti daraja hilo.

Amesema ratiba nyingine zitabaki kama kawaida hadi hapo watakapotangaza vinginevyo. Wanachi waliombwa kuzingatia hilo na kuwaunga mkono ili waweze kuendelean kutoa huduma zao kwa uhakika na usalama unaostahili.


Na Abrahama Ntambara

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search