MAHAKAMANI KISUTU: Watathmini wa almasi, Archard Kalugendo na Edward Rweyemamu wafikishwa mahakamani kwa kuisababishia Serikali hasara..#share

WATATHMINI wa Serikali wa almasi, Archard Kalugendo na Edward Rweyemamu kutoka Wizara ya Nishati na Madini wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashitaka ya kusababisha serikali hasara ya Sh bilioni 2. 4.


Washitakiwa hao ambao ni Mkurugenzi wa Tathmini na Mthamini wa madini, wamesomewa mashitaka mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Respicious Mwijage na Wakili wa serikali, Paul Kadushi.

Kadushi amedai kuwa kati ya Agosti 25 na 31, mwaka huu maeneo ya Dar es Salaam na Shinyanga wakiwa watathmini wa serikali walisababisha hasara ya dola za Marekani 1,118,291.43 sawa na Sh bilioni 2,486,396,982.

Kadushi amedai upelelezi wa shauri hilo haujakamilika wanaomba tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa.

Hakimu Mwijage amesema washitakiwa hawatakiwi kujibu chochote hadi DPP akiamua liendelee mahakamani hapo au la.


Pia amesema masuala ya dhamana sheria kama zilivyo inafikiriwa na mahakama Kuu hivyo mawakili watafuatilia.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search