Breaking: Lissu atoka Central Police...Kumuona Kada Chadema wa Chato aliyeko Mahabusu tangu Agosti 21 mwaka huu....#share
Na Mh Tundu Lisu.
Makamanda wote salaam.
Nimetoka Central Police Station Dar muda huu.
Kuna kamanda wetu wa Chato amewekwa mahabusu tangu tarehe 21
mwezi uliopita. Jina lake ni Obadiah Frank Kiko.
Anaelekea ni maarufu katika siasa za mitandaoni na mnaweza
kumwangalia kwenye facebook page yake 'Frank Kiko' au 'Frank K. Kiko.'
Kosa lake linadaiwa la mtandao. Anadaiwa kamsema vibaya Prof.
Kabudi na timu yake ya makinikia.
Alikamatiwa kwao Chato baadae akahamishiwa Geita, Mwanza na,
tangu Ijumaa iliyopita, yuko Central Dar.
Hadi sasa amenyimwa dhamana ya polisi na hajafikishwa
Mahakamani.
Inaelekea kosa limekuwa kubwa zaidi kwa sababu ya connection
ya Chato.
Kuna watu wanafikiria watapandishwa vyeo wakikamata watu wa
CHADEMA, hasa wa Chato.
Kamanda huyu hana mtu anayemfahamu hapa Dar na hana msaada
hata wa chakula.
Nawaombeni makamanda wa Dar mfanye utaratibu wa kumpelekea
chakula mahabusu. Masuala ya uwakili niachieni mimi.
Naombeni mpaze sauti zenu ili Kamanda Obadiah aachiliwe huru
au afikishwe kortini kesho.
Haya matumizi ya hovyo ya mamlaka ya kipolisi tutayamaliza
kwa kuyapigia kelele muda wowote yanapojitokeza.
Wasalaam.




No comments:
Post a Comment