Ofisi ya Msajili wa Hazina yabaini madudu katika utendaji wa Mashirika na Taasisi za Umma..Asilimia 25 haiendani na mipango...#share

OFISI ya Msajili wa Hazina imebaini asilimia 25 ya tathmini ya utendaji wa Mashirika na Taasisi za Umma katika eneo la mipango mikakati haiendani na bajeti zinazoanishwa na mashirika na taasisi hizo kwa mwaka kusababisha kutofikia malengo yaliyojiwekea.



Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Msajili wa Hazina Dk. Oswald Mashindano wakati wa Mkutano wa utiaji saini mikataba ya kiutendaji kati ya ofisi hiyo na mashirika na taasisi hizo zaidi ya 30.

Amebainisha kuwa uchambuzi wa tafiti wa mikataba iliyoingiwa mwaka 2014/15 na mashirika 71 imebaini udhaifu huo unasababisha majukumu na mipango kutokelezeka kikamilifu.

''Ofisi imebaini katika mikataba iliyopita uchambuzi wa taarifa iliyoandaliwa tumeliona hilo ndio ndio maana mikataba hii tunaitilia mkazo katika meaneo ya usismamizi wa rasilimali watu, fedha na utawala bora,'' alisema Dk. Mashindano.

Dk. Masindano amesema hadi sasa mashirika na taasisi 265 zimeshasaini mkataba huo huku akisisitiza kiasi kikubwa cha fedha kinatumika kwenye uwekezaji, manunuzi na malipo ya mishahara.

Ameongeza kuwa mbali na changamoto hiyo uchambuzi umebaini wa taarifa hiyo umebaini viashiria vya utendaji vilivyoanishwa haviwezi kupimika kwa mujibu wa kazi zilizoanishwa na mashirika yaliyokwisha ingia mikataba.

Amefafanua kuwa bado maeneo ya usimamizi wa rasilimali watu, fedha na utawala yapo chini ya asilimia 10 kutokana na kutosimamiwa ipasavyo na kwamba ukusanyaji wa mapato hautiliwi mkazo.

Pia amesema mashirika mengi yalipata asilimia 17 kwenye eneo la utoaji huduma akibainisha kuwa kazi zilizoanishwa na mashirika haziko kwenye mpangilio ya bajeti.

Aliwahimiza watendaji kuzisimamia vyema mashirika na taasisi zao kwenye utoaji huduma bora na kukusanya mapato yatakayoisaidia Serikali kuendeleza miradi yake.

Ameyataja miongoni mwa mashirika na taasisi zilizosaini mkataba huo ni Hospitali ya Taifa ya Muhimbili(MNH) Mamlaka ya Mawasilaino nchini (TCRA), Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), Chuo Kikuu cha Ushirika-Moshi, Shule ya Sheria nchini, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Udsm) na Tume ya Vyuo Vikuu nchini(TCU).

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Anne Makinda amewashauri watendaji wa mashirika na taasisi zilizoingia mkataba huo kutekeleza majukumu yao ili kuchochea ustawi wake.

Na Hussein Ndubikile


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search