Wabunge UKAWA ukiacha kususia wabunge 7 CUF ...Wataja sababu nyingine Kuu iliyowakimbiza Bungeni leo...#share

WABUNGE wanaotokana na Umoja wa Katiba ya Wananchi [UKAWA), wametaja leo sababu ya kutoka kwao nje ya bunge wakati wa uapishwaji wa wabunge saba wa viti maalumu wa Chama cha Wananchi CUF na kusema wamafanya hivyo ili kupinga kutumika na serikali.


Hayo yamebainisha na Mbunge wa Jimbo la Momba Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) David Silinde, amasema kuwa Bunge hilo limekuwa likikandamizi upinzani na pia kutofuata sheria za nchi jamboa ambalo wanaona siyo sawa.

Amesema kutokana na hali hiyo  ndiyo sababu ya wao kuamua kususia zoezi la uapishwaji wa wabunge hao wa CUF.

"Kama ambavyo leo mmetuona hatujaingia wakati wa kuapishwa kwa baadhi ya wabunge na sababu kubwa ya kutoingia ni kwamba tunapinga bunge kutumika na serikali kukandamiza upinzani pili kutofuata sheria za nchi na jambo la tatu na kubwa kuliko yote ni kwamba tunawaunga mkono wabunge wote waliondolewa na hatufurahii,”

“Kuna vitu vikubwa sisi tunekuwa tukichukizwa navyo kama serikali ku- entetain maamuzi katika chama ambacho kipo kwenye mgogoro kwamba unapendelea upande mmoja unaacha upande mwingine" amesema Silende.

Aidha Silinde aliendelea kudai kuwa " Hiyo ndiyo tumekuwa tukipigania siku zote hatutaki bunge kuendelea kutumika tunataka kuwa na bunge imara waone mifano kama ilivyotokea kule Kenya kama mahakama inaweza kusimama peke yake tunataka na bunge letu liendelee kusimama peke yake" amesitiza Silinde


Na Mwandishi wetu

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search