Breaking News: CCM kimetoa kauli juu ya kupigwa Risasi kwa Lissu... Kimelitaka Jeshi la polisi kuwabaini na kuwashughulika haraka wahusika...#share

CHAMA cha Mapinduzi (CCM) kimesema  kimepokea kwa mshtuko mkubwa  taarifa za kushambuliwa Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu Mchana wa leo.


Taarifa iliyotumwa kwa Umma na Katibu wa NEC- Itikadi na Uenezi wa CCM Humphrey Polepole, kimelaani tukio hilo la kikatili na lisilo na utu.

Aidha kutokana na tukio hilo wamelitaka Jeshi la Polisi kuwatafuta, kufanya uchunguzi wa tukio hilo na kuchukua hatua kali za kisheria kwa waote waliohusika na kitendo hicho kisicho cha kibinadamu.

Na Abraham Ntambara

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search