bREAKING nEWS: Uhuru Kenyatta akubali yaishe.....asema amejipanga kurudi kwa Wakenya kuomba kura...#share

RAIS Uhuru Kenyatta amekubaliana
na uamuzi wa Mahakama ya Juu ya Kenya kufuta ushindi wake kutokana na Mahakama
kubaini kuwepo kwa kasoro katika uchaguzi uliopita katika ngazi ya Urais.
Kauli hiyo imekuja
masaa kadhaa baada ya Mahakama hiyo kutengua matokeo, amesema anaheshimu utawala
wa sheria na kusisitiza wakenya kulinda amani ya nchi na kumtaka kila mtu kuwa
mheshimu jirani yake licha ya tofauti walizonazo za kidini, kisiasa na
kikabila.
“Nachukua nafasi hii
pia kumshukuru Mungu, ni yeye alituumba, ni yeye anayemwezesha kila mkenya
kutembea hapa na pale kwa amani, ni kitu kizuri kwa Kenya kuheshimu utawala wa
sheria,” amesema Kenyatta.
Aidha amebainisha kuwa
wapo tayari kurudi tena kwa wananchi kuomba kura zao kwa ajenda za awali
walizojinadi nazo ambazo ni paoja na jinsi watakavyoleta maendeleo ya nchi na
wananchi wenyewe.
Pia amewataka wapinzani
kujipanga katika uchaguzi huo na kueleza kuwa kikundi cha watu wachache
hakiwezi kubadili matakwa ya wakenya zaidi ya milioni 40.
Na Mwandishi Wetu
No comments:
Post a Comment