Dk. Kigwangalla akana kuwa na Ugomvi na Kikwete, adai wahunzi wa maneno kujenga ukuta baina yao....#share

Naibu waziri wa AfyaMaendeleo
ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Khamis Kigwangalla ameeleza kuwa haoni ajabu yoyote kwa Mbunge wa jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete kupinga
mtazamo wake na wala haimanishi kwamba wawili hao wanaugomvi.
Kauli hiyo imekuja baada ya hivi karibuni Dkt. Kigwangalla kuweka ujumbe katika ukurasa wake wa twitter akitoa maoni yake juu ya usaili wa awamu ya kwanza kwa wanaotafuta ajira katika Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) uliyofanyika Agosti 30, 2017 na kupelekea Mbunge Ridhiwani Kikwete naye kutoa maoni yake juu ya hicho jambo ambalo watu wengi walihisi pengine wawili hao wanachukiana kwa namna moja ama nyingine.
Kutokana na mabandiko hayo ndipo Naibu waziri huyo wa afya Dkt.Kigwangalla naye alipoweza
kujitetea kwa upande wake juu ya tukio zima jinsi lilivyotokea.
"Naona wahunzi wa maneno wanaanza kujenga ukuta kati yangu na Ridhiwani
kikwete. Sioni nia mbaya kwenye 'comment' yake na wala sina kinyongo naye!.Siyo
ajabu mimi na mtani wangu Ridhiwani ama mwanaccm yeyote yule kuwa na mitazamo
tofauti kwenye suala la ajira, hiyo haimaanishi tuna ugomvi", aliandika
Dkt. Kigwangalla.
Pamoja na hayo, Dkt. Kigwangalla aliendelea kwa kusema
Pamoja na hayo, Dkt. Kigwangalla aliendelea kwa kusema
"viongozi wa CCM (wenye dola) ni vizuri tukijadili suala
la changamoto ya ajira kwa sababu tuna nafasi ya kushawishi suluhu ndani".
Kwa upande mwingine, Dkt. Kigwangalla amesema katika
changamoto kubwa ambazo viongozi wa leo wanakupambana nazo ni pamoja na suala
zima la ajira.
Na Mwandishi Wetu
No comments:
Post a Comment