Coutinho hana furaha tena Liverpool, dili la kwenda Barcelona la mmwaga machozi...#share
KIUNGO mshambuliaji wa Klabu ya Liverpool Philippe Coutinho
ameshindwa kuzuia hisia zake na ameonekana wazi kuwa na huzuni nyingi baada ya dili
lake la kuhamia Barcelona kushindikana.
Mchezaji huyo wa kimataifa kutoka Brazil amemwaga machozi
akiwa kwenye jukumu la kuitumikia Timu yake ya Taifa kwani alikuwa akihusishwa kwa muda mrefu kuihama Liverpool
katika dirisha la majira ya kiangazi lililofungwa.
Coutinho mwenye umri wa miaka 25 katika kuhakikisha anahamia
Barcelona alipeleka ombi kushinikiza uhamisho huo ambao hata hivyo
haukuwezekana baada ya klabu yake kudai ada ya uhamisho ya paundi milioni 185.
Mbrazili huyo, ambaye
alikubali kusaini mkataba mpya wa miaka mitano Merseyside Januari, yupo na
kikosi cha timu ya taifa ya Brazili akijiandaa kwa mechi ya Jumanne kufuzu
Kombe la Dunia dhidi ya Colombia.
Kwa mujibu wa Mundo Deportivo, kiungo huyo
alionekana mwenye huzuni alipotaarifiwa kuwa ndoto zake za kucheza Camp Nou
zimekufa.
Inaaminika Barcelona walitoa ofa tano kwa ajili ya Coutinho,
ya mwisho kabisa ikiwa ni ofa ya paundi milioni 113 na nyongeza nyingine.
No comments:
Post a Comment