gOOD nEWS: Serikali Kuanzisha Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi...Lengo kuwezesha Wataalamu wa...#share


SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano inatarajia kuanzisha Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi (ICoT) ili kuzalisha wataalamu wa ngazi ya kati wenye ubobezi katika sekta ya ujenzi.





Hayo yalisemwa jana Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Barabara, John Ngowi kwenye kongamano la pili la kujadili hatua zilizofikiwa juu ya uanzishwaji wa Taasisi hiyo.

Ngowi alisema kuwa kuanzishwa kwa taasisi hiyo nchini kutaondoa pengo la uwiano baina ya wahandisi na kada za chini kama mafundi sanifu na mafundi mchundo ambao ndio wasimamizi wa karibu wakati kazi za ujenzi zinapotekelezwa.

“Mpango mkakati wa Wizara yetu pamoja na mambo mengine, unahusisha uimarishwaji wa sera zinazohusu ujenzi kwa kujenga mazingira wezeshi, mafunzo ya ufundi na matumizi ya teknolojia, mkakati ambao utawezesha kutatua changamoto za umahiri na ubobezi inayokabili sekta ya ujenzi,” alisisitiza Ngowi.

Aidha, Ngowi aliongeza kuwa uanzishwaji wa taasisi hiyo itakuwa chachu ya kufikia azma ya Serikali kuelekea uchumi wa kati wa viwanda ifikapo mwaka 2025 kwa kuongeza rasilimali watu ambao ni muhimu katika usanifu, usimamizi, ujenzi na ukarabati wa miundombinu.

Mwenyekiti wa kampuni ya EcomResearch ambayo ni mshauri wa uanzishwaji wa ICoT, Profesa Godwin Mjema alisema mipango ya  uanzishwaji wake uko katika hatua nzuri na umeshirikisha wadau ili kujadili kozi na mitaala itakayotumika kufundishia.
“Sisi kazi yetu ni kushauri na leo tumekutana na wadau kujadili hatua tuliyofikia, wadau watajadili na kukubaliana na tuliyoandaa, wakikubaliana nasi tutakabidhi kwa Wizara ambao ndio wamiliki na wao watawasilisha Baraza la Taifa Elimu ya Ufundi (NACTE) kwa hatua za usajili,” alisema Profesa Mjema.


Kuanzishwa kwa taasisi hii kunatokana na kuongezeka pengo kati ya wahandisi na kada za chini hali iliyotokana na vyuo vingi vya ufundi kupandishwa hadhi kuwa vyuo vikuu katika miaka ya 1990 bila kuanzishwa vyuo vingine vya ngazi ya kati hasa vya ujenzi.








Na Mwandishi Wetu

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search