Itel Mobile Yasherehekea Maadhimisho Ya Miaka 10 Kwa Mafanikio Makubwa...Soma Habari Kamili na Matukio360..#share
ITEL Mobile leo imesheherekea miaka 10 ya kuanzishwa kwake
huku itel ikiwa ni moja ya kampuni vinara kwa ubora Barani Afrika.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo iliyofanyika jijini Dar es
Salaam Makamu wa Rais wa Itel Leslie Ding, amesema katika kipindi cha miaka 10
itel imeonesha nguvu ya mabadiliko tangu kuingia kwenye soko la Afrika kwa
mwaka huu wa 2017.
“Hii ni kutokana nan a baada ya kuanzishwa kwa timu ya watu
wenye ujuzi na moyo wa kufanya kazi. Miaka 10 sasa, itel imekua na imeenea Zaidi
ya nchi 45 duniani kote. Tunaamini kuwa tuna timu imara ambayo hata mafanikio
ya miaka 10 iliyopita ni kutokana na juhudi kubwa iliyofanywa na timu hii,”
amesema Ding.
Aidha ameongeza kuwa katika kipindi hicho itel mobile imekuwa
na mabadiliko chanya ya bidhaa kutokana na kufuata matakwa ya wateja wake.
Ding ameongeza kuwa kampuni hiyo kwa sasa inapendwa na watu
wengi na inamvuto kutokana na bidhaa zao kuboreshwa zaidi kwa ubunifu mkubwa
ambapo wameweza kuongeza wateja mara mbili zaidi barani Afrika na kwamba hadi
sasa wameweza kuuza simu milioni 100.
Amesema pia mafanikio hayo yamechangiwa na kushirikiana na
mastaa wan chi za Afrika kama mabalozi wa kampuni yao na kwamba wamekuwa kiungo
muhimu katika kuleta ufahamu na uelewa kuhusu kampuni hiyo ambayo ni miongoni
mwa kampuni tatu bora barani Afrika.
Aliongeza kuwa wanaposherehekea miaka 10 wanatarajia nguvu
yao ya mabadiliko itakuwa kubwa zaidi na wanaendelea kuliimarisha bara la
Afrika kwa kutoa bidhaa bora zaidi za mawasiliano.
Naye Balozi wa Itel nchini Irene Uwoya ameipongeza kampuni
hiyo kwa ubora wake ulioifanya kuwa miongoni mwa kampuni tatu bora za barani
Afriaka.
Kwa upande mwingine Itel Mobile imezindua simu mpya za kisasa
ambazo ni itel S12 na S32.
Akizungumzia simu hizo Ofisa Masoko wa Itel Saiphon Asajile alisema simu hizo ni
bora na zina kamera mbili za kuweza kupigia selif mbili za picha.
Pia katika hafla hiyo kampuni hiyo imetoa tuzo kwa washirika
ambao wameweza kufanya vizuri katika biashara na kuchangia mafanikio ya kampuni.
Na Abraham Ntambara
No comments:
Post a Comment