Jeshi la Polisi la Laua Majambazi watatu Dar....#share

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limefanikiwa kukamata silaha moja ya bastola aina ya BERRETA maeneo ya Mbuki Chamazi yenye namba A065775Z ikiwa na Risasi tano ndani ya magazine katika kufuatia majibizano ya risasi kati ya akari na majambazi wapatao watano.
Image result for kamanda lazaro mambosasa
Hayo yamebainishwa leo na Kamanda wa Polisi wa kanda hiyo SACP  Lazaro Mambosasa akizungumza na waandishi wa habari, amesema silaha hiyo waliipata baada askari kupata taarifa ya kuwepo kwa njama za majambazi hao watano kufanya uporaji katika maduka ya M-Pesa/Tigopesa katuika eneo hilo, na hatimaye kuweka mtego ambapo askari walifanikiwa kuwaona majambazi hao wakishuka kwenye gari yao kwa ajili ya kufanya tukio hilo.

Mnamo tarehe 13/09/2017 majira ya 21:00hrs huko maeneo ya kwa Mbiku Chamazi tulifanikiwa kukamata silaha moja bastola aina ya BERRETA yenye namba A065775Z ikiwa na risasi tano ndani ya magazine katika majibizano ya risasi kati ya askari polisi na majambazi wapatao watano,” amesema SACP Mambosasa.

Aidha ameeleza baada ya majambazi hao kufika eneo la tukio na kugundua kuwa wanafuatiliwa na askari walianza kufyatua risasi kuwashambulia askari na ndipo askari walipojibu mashambulizi na kufanikiwa kuwajeruhi majambazi watatu kati ya watano huku wengine wawili wakikimbia.

Amebainisha kwamba silaha hiyo ilipopekuliwa kati ya risasi tano zilizokuwa ndani ya magazine moja ilikuwa chemba tayari kwa kutoka huku maganda sita ya silaha hiyo(pistol) yakipatikana eneo la tukio.

Majambazi waliojeruhiwa walifariki dunia baada ya kufikishwa hospitali ya taifa Muhimbili ili kupatiwa matibabu, Msako mkali unaendelea kuwatafuta majambazi wawili  waliokimbia.


Na Abraham Ntambara

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search