sPORTS nEWS: Timu za Ligi Kuu, Draja la Kwanza Hatarini Kutupwa Nje ya Mashindano....#share

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limetaka hadi kufikia Septemba 22 mwaka huu, klabu zote 16 za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) na   24 Ligi Daraja la Kwanza (FDL), ziwe zimekamilisha taratibu za kupata Leseni za Klabu, zikishindwa zitaondolewa katika mashindano.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TFF leo, kupitia kwa Ofisa Habari wake, Alfred Lucas, Kamati ya Leseni za Klabu imebainisha kuwa timu tano za Ligi Kuu ya VPL  kati ya 16 hazikuchukua fomu za maombi ya Leseni za klabu, huku 11 zikichukua na kurejesha lakini zina upungufu mkubwa katika kukamilisha vigezo.

Kamati ya Leseni za Klabu imekutana zaidi ya mara tatu katika vikao na kujiridhisha kwamba kwa ujumla vigezo vifuatavyo havijakamilika kwa asilimia 100 katika klabu nyingi kama zifuatavyo:

1. Klabu zote hazina programu ya kuendeleza mpira kwa vijana.

2. Taarifa za klabu haielezi kuhusu miundombinu ya kuhudumia walemavu wakati wa mchezo.
3. Klabu hazijaonesha uwanja wa mazoezi.

4. Hazijaambatanisha mikataba ya watendaji kama vile Katibu Mkuu; Ofisa Usalama wa timu, Mhasibu au mkurugenzi wa fedha, na daktari n.k.

5. Taarifa hazina maelezo ya kocha wa timu za vijana.
6. Klabu hazijajaza  fomu za kuomba Leseni ya klabu.
7. Hazijambatanisha katiba ya klabu.

8. Klabu hazijaambatanisha ripoti ya fedha ya mwaka.
9. Klabu hazijajaza fomu ya kuthibitisha kushiriki mashindano ya Ligi Kuu ya Vodacom.

Taarifa hiyo imesema, Kamati ya Leseni ya Klabu inazitaka klabu kukamilisha vigezo hivyo kabla ya Septemba 22, mwaka huu. Vinginevyo, klabu  inaweza kuondolewa kwenye mashindano.

Na Mwandishi Wetu

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search