Kamanda Mambosasa aweka hadharani sababu kumshikiria Rungwe kwa siku 9...Aachiwa kwa dhamana Usiku mnene...#share
POLISI
Kanda Maalim Dar es Salaam imeeleza sababu za kumshikiria mgombea urais katika
Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, Hashim Rungwe ambaye jana aliachiwa kwa dhamana
baada ya kusota mahabusu kwa siku nne.
Mwanasiasa
huyo ambaye ni mwenyekiti wa Chama cha Ukombozi wa Umma (Chaumma), alishikiriwa
kwa siku tisa akituhumiwa kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.
Akizungumza
na waandishi wa habari leo Kamanda wa Polisi Kanda hiyo, Lazaro Mambosasa amesema polisi ilimkamata
mwenyekiti huyo wa Chaumma tangu Agosti 28 baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa mlalamikaji Suleiman Ysian (48) na mwezake Ali Riza Belgen
ambao ni mfanyabishara na Raia wa Uturuki aliyefika nchini kwa biashara ya
kununua korosho.
“Raia
hao wa kigeni walielezea jeshi la polisi
nia yao ya kununua korosho kiasi cha tani 15 kwa mwenyeji wao Salum
Mohamed ambaye aliwahakikishia kuwa kampuni yake inauwezo wa kuwauzia, na
kuandaa mkataba na kampuni ya Les tropiques group mining sprl limited” alisema.
Amesema
baada ya makubaliano hayo muuzaji huyo
wa korosho aliwajulisha kumshirikisha wakili wake katika makabidhiano hayo ya
fedha, ambapo walikwenda hadi kwa wakili Rungwe ambaye alishuhudia makabidhiano
hyo.
“Muuzaji
alimtaka mteja wake atume malipo ya awali ya kuaandaa korosho kupitia Benki ya
CRDB kwa kutumia akaunti ya wakili wake Hashimu Rungwe, kiasi cha USD 72,000 sawa
na sh.milioni 160 za kitanzania, ambazo zingelipwa kwa awamu tatu na mwisho
mzigo ambapo ungefika wangemalizia asilimia 60” alieleza Kamanda
Mambosasa.
Amesema kuwa mfanyabiashara huyo akiwa
Uturuki Novemba 22, 2016 alituma fedha kiasi cha zaidi ya sh.milioni
20 kwenye akaunti ya Wakili na sh.milion mbili
kama gharama za kwenda Lindi kuhakikisha mzigo kama hupo.
Hata
hivyo baada ya uthibitisho huo kutoka mtuhumiwa huyo Novemba 12, mwakajana
alitumiwa kiasi cha zaidi ya sh.milion 30 katika akauti ileile, hivyo mteja alipoona gharama zinazidi
kuwa kubwa na hakuna mzigo alimua kurudi Uturuki akisubili kutumiwa.
Na Mwandishi Wetu




No comments:
Post a Comment