Ona jinsi TECNO inavyoendelea kutoa burudani ya SPARK kwa watanzania katika mitaa mbalimbali nchini...Kilele chake kuwa jijini Mwanza kwa washindi kuta.....#share
SHINDA TECNO SPARK MTAANI KWAKO.
KAMPUNI ya simu ya TECNO imekuja kivingine kwa kuwaletea
wateja wake na wanatanzania kwa
ujumla burudani ya SPARK katika mitaa
mbalimbali ya majiji yanayopatikana nchini Tanzania.
Mikoa ya Dar es salaam, Morogoro na Tanga imekua ya kwanza
kushuhudia michezo mbali mbali ya
kuvutia inayoletwa na TECNO katika mitaa mbalimbali ya mikoa hiyo ikiwa na
madhumuni makubwa ya kuwapa burudani wateja wao na kuitambulisha simu mpya
kabisa ya TECNO SPARK.
Watoa burudani hao wa TECNO wanapita katika mitaa mbalimbali
ikiwemo kihonda, kichangani, msamvu katika mkoa wa morogoro huku maeneo kama
mabanda ya papa, magomeni, muheza, pongwe na korogwe mkoani Tanga yakiwa katika
mtiririko wa kutembelewa na burudani
hizo kabambe kutokea TECNO.
TECNO inawapa nafasi wanatanzania wote popote walipo
wanachotakiwa kufanya endapo wataliona basi la kampuni ya TECNO likiwa
limeandikwa TECNO SPARK, wajiunge popote pale ambako burudani zitakua
zinatolewa katika mitaa yao hivyo wataweza kujishindia zawadi za aina
mbalimbali ikiwemo simu mpya kabisa ya
TECNO SPARK..
TECNO SPARK ni moja
kati ya matolewa bora mapya ya simu kutokea TECNO yanayofanya vizur sokoni kwa
kupendwa watanzania wengi kutokana na sifa zake kwani ina kamera nzuri ya 13mp nyuma , pia ina teknolojia ya usalama
wa vidole huku umbo lake likiwa ni kuvutio kikubwa katika macho pale ambako
mtumiaji anakua ameishika mkononi. Kioo chake ni 5.5 inchi, 16 gb za kuweka
vitu ndani pamoja na 2 gb ram.
Burudani hizi za TECNO zitakua na kilele chake katika ukumbi
wa burudani wa club Rock bottom mkoani Mwanza, ambapo wapenzi kampuni ya TECNO
Mobile watatangazwa walioweza kujishindia zawadi mbalimbali ikiwemo simu mpya
ya SPARK.
Bado hujachelewa
mkoani Morogoro, Tanga, Arusha, Manyara pamoja Mwanza unaweza kupiga picha
endapo utalion basi la TECNO SPARK au burudani katika mtaa wako alafu weka katika mitandao yako ya
kijamii aidha Facebook, twitter au Instagram ukiandika #vimbanaspark ili uweze
kujishindia zawadi kemkem kutokea TECNO.



No comments:
Post a Comment