Chadema Kimelituhumu Bunge kuvunja Katiba kwa Kuomba Fedha za Ziada Nje ya....#share
CHAMA
cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimedai Bunge limevunja Katiba kwa kuomba
fedha za ziada nje ya bajeti yake iliyoidhinishwa na Bunge bila kupitisha
maombi bungeni.
Akizungumza
na waandishi wa habari leo Katibu Mkuu wa chama hicho, Vicent Mashinji alisema ibara
ya 135 (2) inaeleza kuwa Fedha ambazo hazijawekwa kwenye mfuko mkuu wa Hazina
ya serikali ni zile zote ambazo zimetajwa na sheria kwamba zitumike kwa
shughuli maalum au ziwekwe katika mfuko mwingine kwa ajili ya matumizi maalum.
“Kwa
mujibu sheria ya uendeshaji wa Bunge mwaka 2008, kifungu cha 31 kinaeleza kuwa
fedha zote kwa ajili ya uendeshaji wa bunge zinawekwa kwenye mfuko maalum
wa bunge kama ulivyoanzishwa na sheria hiyo na usimamizi mkuu wa fedha hizo ni
Katibu wa Bunge kwa mujibu wa kipengele cha (2) na (3),” amesema.
Amesema
kati ya June 21, 2017 na Agosti 15, 2017 Katibu wa Bunge aliandika barua tatu
tofauti akiomba fedha zaidi ya Sh bilioni 9 kwa waziri wa Fedha na kwa Katibu
Mkuu Hazina kwa ajili ya kugharamia bajeti ya ziada na matumizi mengineyo kwa
ajili ya bunge ikiwa ni nje ya bajeti iliyoidhinishwa 2016/17.
Dk.
Mashinji amesema tangu wakati huo mpaka Agosti 15 serikali ilishatoa bajeti ya
ziada kwa bunge sh. Biloni 7 kutoka katika mfuko mkuu wa hazina bila kufuata
masharti ya katiba na kwmaba inategemewa kuwa itaendelea kutoa sh. Bilioni 2.5
kwa ajili ya kulipia gharama za posho ya jimbo ya Juni mwaka 2017 ambayo
haijalipwa kwa ukamilifu.
Fedha
zilizotolewa kama bajeti ya ziada zilitumika kwenye kukidhi mahitaji ya
kulipia posho mbalimbali za wabunge ya Juni mwaka 2017, posho za vikao kwa
wabunge ya Mei na Juni mwaka jana posho ya masaa mengi kwa watumishi ya Mei na ya
kikao kamati maalum.
Amefafanua
kuwa katika mwaka wa fedha wa 2016/17 Bunge liliidhinisha fedha kwa ajili ya
matumizi ya kawaida sh. Bilioni 92 ambapo mishahara ni sh. Bilioni 23, matumzi
mengineyo sh. Bilioni 68 na miradi ya maendeleo ya fedha za ndani sh. Bilioni
7.
Amesema
kwa mujibu wa katiba ya nchi pamoja na sheria na kanuni zinazoongoza bunge na
serikali ni kuwa bunge linaisimamia Serikali.
Amesema
sheria ilitungwa ili bunge liwe na fedha zake kwenye mfuko maalum likiwa kama
mhimili unaojitegemea na unaopaswa kujiendesha bila kuwa tegemezi.
Na Mwandishi Wetu




No comments:
Post a Comment